Thursday 22 March 2012

KURUNZI YA KANISA FM...2

HABARI YA KANISA FM
Asanti sana kwa kujiunga nasi tena tunapomulika  yaliyojiri katika nyanja za kiroho. Nina mengi niliyokwandalia leo lakini kawaida ni kama sheria… Vimulimuli kwanza.
VIMULIMULI
-Vijana wasiwe wavivu…
-Hakuna limshindalo Mola…
-Mchezaji Daudi aweka rekodi mpya ya Tenisi… na
-Wanafunzi watunukiwa.
Hujambo na karibu kwa habari timilifu. Mimi ni Paul King’ori.
HABARI TIMILIFU
   Waziri wa maswala ya vijana na Werevu Profesa Suleimani leo amewaasa vijana dhidi ya uvivu na ulegevu. Huku akipigia mfano wa shamba la mtu mvivu alisema shamba hilo hujawa na miiba na ua wake huwa umeanguka. Akizungumza na Kanisa FM Profesa Suleimani aliongeza kuwa watu wavivu huvamiwa na umaskini kama jambazi. Kwa habari zaidi tumia anwani ifaatayo ya mtandao Proverbs @ Bible. 24:30.co.ke Waziri alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika ziara zake za magatuzi.
  HABARI KUTOKA BUNGE
   Mbunge maalumu malaika wa Mungu leo alimhimiza waziri wa injili Mheshimiwa Luka ajibu swali na azungumzie swala lalilozua utata katika katiba hususan wakati huu ambapo kunazo harakati za kuitekeleza katiba mpya.
Swali hilo lililo katika kitabu cha Sheria cha Mwanzo 18:14 linauliza “Je, kuna jambo ngumu zaidi kwa Mungu?”
Mheshimiwa Luka aliye pia ni mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Binguni ya Uenezaji wa Injili alisimama kwa idhini ya Spika na kulijibu swali hilo kwa kifupi lakini kwa uhalisi ufaao. Akirejelea ripoti aliyokuwa ameitoa hapo awali iliyojulikana kama ‘The Luke Report,’ iliyonukuliwa kutoka kitabu cha Luka 1:37 alisema kuwa hakuna jambo lisilowezekana na Mwenyezi Mungu. Hii ni Ripoti iliyonuiwa kuwapa motisha wale wote ambao hawajafanikiwa kufikia kiwango kihitajikacho ili watunukiwe, basi wasife moyo kamwe, watie bidii na wamtumainie Mungu.
KURUNZI MICHEZONI
Hapo jana mchezaji mashuhuri wa Tenisi Daudi alijinyakulia ushindi kwa mara ya Tano mfululizo dhidi ya Mfilisti. Daudi aliyemshinda Goliathi kwa pointi 70-02 alijishindia taji la mchezaji bora duniani. Daudi pia ndiye mchezaji mchanga mno kumshinda Bingwa mtetezi wa Waflisti, Goliathi. Daudi alipata ushindi baada ya kumuua Goliathi aliyekuwa akiwabeza wana wa Israeli kila uchao. Kutoka kanisa Fm tunampongeza Daudi na sifa zimwendee Mungu wa Isaka na Yakobo.
HALI YA ANGA
Leo hali ya anga imebadilika kidogo katika Shule ya Upili ya Kairo maanake kuna mchanganyiko wa rangi. Haya ni matokeo ya halaiki kubwa iliyohudhuria  na ni tofauti na ile rangi ambayo imezoa macho, yaani rangi ya sare nyekundu. Pia nyusi za joto zitakuwa juu kidogo kwa furaha ya wanafunzi kwa kutembelewa na wazazi na wageni wengine na la muhimu zaidi kutunukiwa.
Basi kwa watakaotunukiwa-Pongezi na Hongera nyingi kutoka Kanisa FM. Kwa wale hawajabahatika, kuna kesho utie bidii… Mwelekezi wangu ananiarifu kuwa wakati umenitia mikatale, sina budi kuondoka. Hadi siku nyingine, barikiwa. Mimi ni Paul King’ori.  

No comments:

Post a Comment